BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, March 16, 2013

TSJ yang'ara mashindano ya Utangazaji 2013




Frank Aman, Mwananchi
Dar es Salaam. Chuo cha uandishi wa habari cha Time School of Journalism (TSJ) kibeibuka kidedea kwa kupata alama za juu katika vipingele vyote katika mashindano ya utangazaji yaliyohusisha vyuo vya uandishi wa habari yaliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Vipengele ambavyo vilikipatia ushindi chuo hicho ikiwa ni mara ya pili kupata ushindi huo tangu mashindano hayo yaanzishwe mwaka 2011 vilikuwa ni pamoja na uchambuzi wa magazeti, Kusoma taarifa ya habari, kuendesha vipindi maalum, Michezo pamoja na vipindi vya burudani.
Akizungumza mara ya baada ya kutangazwa washindi, Rais wa chuo hicho Bi Frida Matinya alisema kuwa licha ya maandalizi ya muda mfupi kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wao ushindi huo umepatikana kutokana na mafunzo waliyoyapata chuoni hapo pamoja na vipaji vya wanafunzi walioshiriki katika mashidano hayo.
Alisema kuwa asilimia kubwa ya washiriki katika shidano hilo walio wakilisha chuo hicho wengi wao walikuwa ni wanafunzi walioingia muhula wa kwanza mwaka huu hivyo hali hiyo imedhihilisha vipaji na uwezo wa wanafunzi binafsi.
“Toka kuanza kwa shindano hili mara zote tumeibika kidedea kwani mwaka 2011 lilipoanza shindano hili ambalo lilifanyika katika chuo cha uandishi wa habari cha Royal College of Tanzania (RCT) tulikuwa washindi wa kwanza, mwaka jana yalifanyika chuo cha uandishi wa habari cha Mlimani eneo la Mbezi tulikuwa washindi wa pili,” alisema na kuongeza;
“Hii pekee imedhihilisha kuwa kuwa wanafunzi wa chuo hiki wana uwezo mkubwa katika fani ya utangazaji na pia taaluma inayotolewa katika chuo chetu inakidhi vigezo vya sisi kuingia katika ushindani wa aina yoyote hata katika ngazi ya ajira.”

Bi Matinya alisema kuwa katika shindano hilo chuo cha RCT kimekuchukua nafasi ya pili na nafasi ya tatu ikishikwa na chuo cha Dar es Salaam City College (DACISO).
Mashindano hayo yalifanyika katika viwanja vya TSJ maeneo ya Ilala Sharifu Shamba yalijumisha idadi ya vyuo sita (6) lakini vyuo ambavyo vilishiriki jana katika kinyang’anyiro hicho ni vitatu ambavyo ni RCT, DACICO pamoja na TSJ.

Wakiongee na Mwananchi baadhi ya wanafunzi wa Tsj walisema “ sisi ndio sisi ushindi kwetu daima kwani tulijiandaa vya kutosha japokuwa muda tuliyofanya mazoezi ni mdogo mno ila tumestahiki kuwa washindi wa nafasi ya kwanza”
MWISHO.

Sunday, January 20, 2013

Delyla-My Salvation

Saturday, December 29, 2012

Miaka 51 baada ya uhuru wawekezaji wanaongezeka tuu

 Hapa sio Mkoani Simiyu bali ni Dar wawekezaji kibao lakini maisha bado kitendawili... kwa kiasi mji unakua atiii!!!



Tuesday, December 18, 2012

Vodacom Family Day..

 Meneja wa  matangazo wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Bw Nicholas Machugu (Kushoto) akikabidhi kombe kwa nahodha wa timu ya wa mpira wa miguu kutoka idara ya biashara kwa nahodha wa timu ya idara ya biashara katika tamasha la Vodacom Family day lililofanyika katika viwanja vya kunduchi Beach Hotel lililofanyika Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Waimbaji wa Skylight Band wakitumbuiza katika tamasha la Vodacom Family Day, tamasha lililo fanyika katika viwanja wa Kunduchi Beach Hotel mwishoni mwa wiki.

Monday, December 17, 2012

Wafanyakazi wa Vodacom watoa msaada kwa kituo cha yatima Friend of Don Bosco Kimara

 wafanyakazi wa mtandao wa simu ya mkononi Vodacom Tanzania kitengo cha Customer care wakitoa msaada wa vitu mbali mbali kama vyakula, vitanda, magodoro vyenye thamani ya Sh6 million.

Saturday, November 24, 2012

Msanii wa Filamu Tanzania John Maganga afariki

John Maganga
Marehemu John Maganga mwigizaji wa filamu enzi za uhai wake.
KATIKA Tasnia ya filamu Swahiliwood wiki hii imekubwa na simanzi baada ya wasanii wake kuaga Dunia siku ya jana msanii mahiri wa maigizo Halid Mohamed ‘Mlopelo’ alizikwa na leo hii tasnia hiyo imekubwa na msiba mwingine mkubwa baada ya John Maganga kufariki katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
John Maganga
Marehemu John Maganga akiwa na msanii mwenzake katika moja ya sene.
John Maganga
Marehemu John Maganga enzi za uhai wake.
Taarifa za awali zinasema kuwa marehemu John amefikwa na mauti baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa tumbo, ni huzuni kwa wasanii na wadau wa tasnia hiyo ya filamu kwani wengi wamedai kuwa msanii huyo ni jana tu walikuwa naye katika matembezi na leo hatunaye tena.
Taarifa zaidi kuhusu mazishi mtazipata hapa hapa bado timu ya FC inajaribu kufuatilia kwa karibu na kuwataarifu, Bwana Mungu alitoa na ametwaha jina lake lihimidiwe.

Friday, October 26, 2012

KITU KIPYA KUTOKA D PRODUCTION "MAGIC MONEY"


""zimebaki sikuchache kuingia sokoni noma...""
ni kauli ya msanii wa filamu Daudi Michael katika wall yake ya facebook akiongelea ujio wa fila mu yake mpya ijulikanayo kama Magic Money iliyoandaliwa na D Production na wasambazaji ni Pili Pili entertainment.... JIPATIE NAKALA YAKO COMING SOOOOON!!!!! BIGUP D PROD....

Sunday, September 2, 2012

TSJ Bash ilivyo wabamba wanafunzi...

 Hao ni washiriki mashindano ya kumtafuta Miss na Mr Tsj kwa mwaka 2012/2013 yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Mbalamwezi Beach na hapo wakiwa wanaingia katika steji.
 Wakiwa katika katika steji wakiwa burudisha wanafunzi wenzao kutoka chuo cha uandishi habari kiitwacho Tsj kilichopo Ilala-Sharifu shamba pamoja na Mkuu wao wa chuo cha TSJ akiwa bega kwabega akiongozana na mgeni Rasmi kutoka kitengo cha Haki za kibinaadamu{LHRC}
                                            Washiriki wa MISS na MR TSJ wakiwa katika picha ya pamoja hapo
 Picha ya pamoja wakiwepo washindi wa MISS na MR TSJ kwa mwaka huu, wakiwa pamoja  na mkuu wa chuo upande wa kulia aliyevaa nguo ya rangi nyeupe Bi Carolyne Setumbi kushoto Rais wa serikali ya wanafunzi ya TISJOSO Bi Frida Matinya.
 Picha ya pamoja wakiwepo washindi wa MISS na MR TSJ kwa mwaka huu, wakiwa pamoja  na mkuu wa chuo upande wa kulia aliyevaa nguo ya rangi nyeupe Bi Carolyne Setumbi kushoto Rais wa serikali ya wanafunzi ya TISJOSO Bi Frida Matinya.pamoja na Miss na Mr ambao wamewavalisha Taji washindi wa mwaka huu.

Sunday, August 12, 2012

TAMASHA LA DINI "LOVE TANZANIA" LILIVYOTIA FORA VIWANJA VYA JANGWANI JIJI DAR.


Pichani Juu na Chini ni Umati wa Watanzania uliofurika kwenye Tamasha la Dini lililopewa jina la LOVE TANZANIA linaloendelea katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam likiongozwa na Askofu Andrew Palau kutoka Marekani.
Vijana walioongoza na Askofu Andrew Palau wakitoa burudani na mafundisho ya dini kwa njia muziki.
Wana Dar es Salaam wakiendelea…

Saturday, August 11, 2012

MRITHI WA TAJI LA MISS &MR TSJ KUJULIKANA AUGUST 25 MWAKA HUU





SERIKALI  ya wanafunzi ya chuo cha uandishi wa habari cha Time School of Journalism (TSJ) inatarajia kuwapata wawakilishi wapya wa taji la Miss na Mr TSJ katika sherehe za ‘Bash’  ambazo zimelenga kuwakaribisha wanafunzi wapya wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho.
Sherehe hizo ambazo zinatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi August tarehe 25 zitafanyika katika uwanja wa Mwalamwezi Beach, na itasindikizwa na wasanii mabli mbali wa muziki wa Bongo flava.
Akizungumza na gazeti hili, Rais wa chuo hicho Bi Frida Matinya alisema kuwa sherehe hizo ni moja ya utaratibu waliojiwekea katika kuwapokea wanafunzi wapya ambao ni wameingia chuoni hapo kuchukua kozi mabli mbali.
Alisema kuwa katika sherehe hizo ambazo zitashereheshwa na michezo mbali mbali ikiwa ni pamoja na maonyesho ya mavazi, Mr na Miss TSJ, Kuimba, kuvuta kamba, kuogelea na michezo mingine mingi ya baharini.
“Lengo la sherehe hizo ni kuwa kawaweka karibu wanafunzi wageni na pia kufahamiana pamoja na kujenga mazingira rafiki kwa wanafunzi wote pia kuwapa burudani pia kujijenga kisaikolojia kwani michezo hujenga, kujumuika pamoja katika hafla hii itatuwezesha kuwa na ushirikiano wa kutosha,” alisema.
MWISHO.