BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Saturday, August 11, 2012

MRITHI WA TAJI LA MISS &MR TSJ KUJULIKANA AUGUST 25 MWAKA HUU





SERIKALI  ya wanafunzi ya chuo cha uandishi wa habari cha Time School of Journalism (TSJ) inatarajia kuwapata wawakilishi wapya wa taji la Miss na Mr TSJ katika sherehe za ‘Bash’  ambazo zimelenga kuwakaribisha wanafunzi wapya wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho.
Sherehe hizo ambazo zinatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi August tarehe 25 zitafanyika katika uwanja wa Mwalamwezi Beach, na itasindikizwa na wasanii mabli mbali wa muziki wa Bongo flava.
Akizungumza na gazeti hili, Rais wa chuo hicho Bi Frida Matinya alisema kuwa sherehe hizo ni moja ya utaratibu waliojiwekea katika kuwapokea wanafunzi wapya ambao ni wameingia chuoni hapo kuchukua kozi mabli mbali.
Alisema kuwa katika sherehe hizo ambazo zitashereheshwa na michezo mbali mbali ikiwa ni pamoja na maonyesho ya mavazi, Mr na Miss TSJ, Kuimba, kuvuta kamba, kuogelea na michezo mingine mingi ya baharini.
“Lengo la sherehe hizo ni kuwa kawaweka karibu wanafunzi wageni na pia kufahamiana pamoja na kujenga mazingira rafiki kwa wanafunzi wote pia kuwapa burudani pia kujijenga kisaikolojia kwani michezo hujenga, kujumuika pamoja katika hafla hii itatuwezesha kuwa na ushirikiano wa kutosha,” alisema.
MWISHO.


No comments:

Post a Comment