BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

Promo

Promo

Friday, October 28, 2011

WASAMBAZAJI WANAZINGUA ASEMA ROSE...


MTAYARISHAJI na mwigizaji nyota wa filamu wa Bongo, Rose Ndauka, amesema kuwa filamu yake ya Diary imeshindwa kuingia sokoni mapema kwa sababu ya matatizo ya usambazaji.

Badala yake ameamua kuigiza filamu ya Ruben n� Angel wakati akijaribu kumtafuta msambazaji anayefaa.

Filamu ya Diary ilikuwa itoke mapema kabla ya filamu ya Ruben n� Angel, lakini kutokana na matatizo ya usambazaji ameamua kusitisha zoezi hilo. 


Mwanadada huyu ambaye anamiliki kampuni yake inayojulikana kwa jina la Rose Ndauka Entertainment, anatayarisha filamu zake mwenyewe pia na kushiriki filamu nyingine.

�Nilikuwa nimewaahidi wapenzi wa kazi zangu kuwa filamu ya Diary inatoka mwezi huu, na watu walikuwa wanasubiri kwa hamu itoke, lakini ratiba imebadilika badala yake nimetoa filamu nyingine ya Ruben n� Angel,� alisema Ndauka.

Filamu ya Ruben wameshiriki wasanii kama Khaleed Tajiri, Irene James, Ndauka na wasanii wengine filamu hiyo ipo mtaani ikiendelea kuuzwa.


Saturday, October 15, 2011

Aunt Ezekiel asema hajafungiwa...


BAADA ya uvumi wa kufungiwa kwa mwigizaji Aunty Ezekiel kuenea , mwenyewe amefunguka na kusema kuwa huo ni uvumi tu ambao hata yeye amekuwa akiusikia tu bila kujua chanzo chake.

“Sijui nani aliyeanzisha habari hizi, lakini mimi sijafungiwa na sasa ninapozungumza na wewe nipo mzigoni nikiandaa filamu yangu mpya ambayo nitaiingiza sokoni muda si mrefu,” alisema Aunty.

Aunty amesema filamu yake hiyo itaitwa House Boy and House Boy na itakuwa ikielezea maisha ya kila siku ya wafanyakazi wa ndani.

Mwenyekiti wa Bongo Movie, Jacob Steven amesema umoja wao huo haukumfungia kuigiza, bali asingeruhusiw akufanya kazi na msanii yoyote wa umoja huo.

Hata hivyo alisema Aunty ameshajirekebisha kwahiyo anaweza kuendelea na kazi kama kawaida.

Hata hivyo kufungiwa kwa Aunty kuna leta utata kutokana na waigizaji kuwa na vyama mbalimbali ambvyo mpaka sasa hakijukani kipi chenye nguvu ya kuweza kumfungia msanii.

Kipindi cha nyuma kulikuwa na shirikisho la wasanii wa filamu TAFF ambalo inasemekana liliundwa baada ya serikali kuamuru uundwe umoja utakaowawakilisha kwenye shughuli mbalimbali.

Baadae ukaundwa umoja huu uitwao Bongo Movie ambao wasanii wengine wanadai kutoutambua kutokana na mazingira yake nakusema kuwa umeundwa kwaajili ya maslahi ya wasanii wachache.

Saturday, October 1, 2011

Kitu Kipya kabisa kwenye game...

 
RATIFA MTOBI (TANITA)
Amezaliwa Tanga miaka kumi na tisa iliyopita. Mwigizaji wa Tuesday Entertainment. anapendelea kuogelea na riadha.
 
Ni Mwanadada Chipukizi ambaye yuko pamoja na actors wengine katika tamthiliya ya Millosis inayorushwa TBC1 kutoka kwa Director Tuesday Kihangala.

Shirley; Nyota anayetikisa kwenye tamthiliya ya Millosiss...


Jina halisi la chipukizi huyo ni Celina Victor, lakini mashabiki wa filamu wanamfahamu kwa 'Shirley', msanii ambaye aliweza kuonesha uwezo katika tamthilia ya 'Jumba la Dhahabu'.
Nyota huyo anajitahidi kusaka umaarufu lakini bado ana changamoto nyingi za kucheza filamu ambazo zitazidi kumweka juu kama ilivyo kwa The Sandy kazi ambayo inafanya vizuri.


Katika mawasiliano na mdada huyu na blog hii kupitia mtandao wa Facebook Shirley alifunguka na kutaja kazi mbali mbali ambazo aliwahi kufanya na bado zingine zinazotarajiwa kutoka hivi karibuni.


“Kazi nilizowahi kucheza ni jumba la dhahabu (series) + movies nilizoshiriki kuna mboni yang ya kina sajuki, zingine indecency, jasho la kifo, hostell na XXL ambayo haijatoka bado. Also nipo kwny drama inaitwa millosis inaruka Tbc kwa sasa,” alisema Shirley.